Thursday, February 23, 2012

Mtumishi Freddy Chavala Kuanza Season One Ya Matamasha ya Cheka Tena(Laugh Again Concert ) Tar 4 March 2012,Pale Landmark Hotel,Ubungo,Dsm.


Crown Chavala
Baada ya mafanikio makubwa ya uzinduzi wa matamasha ya Cheka Tena mwishoni mwa mwaka jana, Nov 20 2011 pale Crystall hall ya Blue pearl hotel, Ubungo plaza. Sasa mbeba maono wa Matamasha hayo Mtumishi Freddy Chavala ameamua kuanza rasmi MSIMU WA KWANZA(SEASON ONE) wa matamasha hayo ya stand up comedy Tanzania, na Tamasha la kwanza la LAUGH AGAIN CONCERT mwaka huu litakalofanyika pale Ibungira hall katika ukumbi wa  LANDMARK HOTEL Ubungo river side, jumapili ya kwanza ya march(4th March 2012), kuanzia saa nane na nusu mpaka mbili usiku(2:30pm-8pm). 

Mbali na CROWN CHAVALA,Tamasha hili la Ubungo litawapandisha comedians chipukizi watano ambao ni Senior ABBY, Gerald Mrema, Richard Chidundo, Josephine Lukweto na MC MANU a.k.a Pilipili ya Sherehe toka Dodoma,Makundi mengine ya watu watakaonogesha tamasha hili ni pamoja na kundi maarufu la vijana waimbaji waitwao GLORIOUS CELEBRATION BAND, pia DAR ES SALAAM GOSPEL BAND, VOCAPELLA GROUP, VICTOR ARON,MADAM RUTH &CHRISS na wengine wengi bila kusahau kundi la DANCE.

Glorious Celebration watakuwepo Landmark Hotel wakimsindikiza Chavala
LAUGH AGAIN CONCERT One One litahusisha Stand Up Comedy(Zaidi), pamoja na Acapella, Dance,Sebene,Story telling, Zawadi & Suprises, Open Mic,Drama,na mengine mengi yatokanayo! Mbali na hayo kutakuwa na uzinduzi wa FORUM iitwayo QUALITY-LOVE.com, ambayo itakuwa maalumu kwa ajili ya kujadili maswala ya Upendo safi kwa kina,ubora,upana na ubora wake katika nyanja mbalimbali za maisha ya binadamu. Na kama mambo yataenda kama yalivyopangwa kutazinduliwa kitabu kiitwacho “NO MORE SCHOOL FOR YOU”(Your birth was your Graduation) By FREDY E. CHAVALA.

Kiingilio kwa tamasha hili itakuwa 5000/= kwa tiketi, ambazo zinapatikana Victory Christian Centre(VCC);Tarakea Restaurant(Mwenge),Silver Spoon and Tausi Fashion pale Mlimani City,Global Publisher na Praise Power Radio
Lakini pia mtu anaweza kununua tiketi kwa M-Pesa (0753 883 797) au Tigo Pesa (0713 883797) kwa kutuma 6000/= na atapata tiketi yake mlangoni, lakini hakikisha unatuma pesa kwa namba yako mwenyewe iliyosajiliwa kwa jina lako!

LAUGH AGAIN CONCERT Season One itakuwa na matamasha nane katika mikoa mitano ya hapa nchini kwa kuanzia, Matamasha haya yatafanyika kuanzia March-August/September 2012 katika mikoa ya Dar es salaam(3),Arusha(1),Mwanza(1),Dodoma(2) na Mbeya(1).
Tar 1st April ni ARUSHA 
29th April ni ndani ya COLD CREST HOTEL,Mwanza 
then DSM tena !



 By Crown Chavala,The King of Standup Comedy! Alimaarufu kama President Chavala!

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...